John 18:3-8
3 aHivyo Yuda akaja bustanini. Aliongoza kikosi cha askari wa Kirumi, na baadhi ya maafisa kutoka kwa viongozi wa makuhani na Mafarisayo. Nao walikuwa wamechukua taa, mienge na silaha. 4 bIsa akijua yale yote yatakayompata, akajitokeza mbele yao akawauliza, “Mnamtafuta nani?” 5 cWao wakamjibu, “Isa Al-Nasiri.” Isa akawajibu, “Mimi ndiye.” Yuda, yule aliyemsaliti alikuwa amesimama pamoja nao. 6Isa alipowaambia, “Mimi ndiye,” walirudi nyuma na kuanguka chini! 7 dAkawauliza tena, “Mnamtafuta nani?” Nao wakamjibu, “Isa Al-Nasiri.” 8Isa akawaambia, “Nimekwisha kuwaambia kuwa, mimi ndiye; kwa hiyo kama mnanitafuta mimi, waacheni hawa watu waende zao.”
Copyright information for
SwhKC